Gideon Moi apoteza kiti cha useneta Baringo

Cheptumo alishinda kwa kura 141,777 huku Moi akiiuka wa pili kwa kura 71,408.

Muhtasari

•Gideon Moi amepoteza kiti chake baada ya William Cheptumo kutangazwa mshindi katika kinyang'anyiro cha mwaka huu.

• Gideon alikuwa na ugumu wa kueleza kwa nini anapata kura na kutoweka mara moja badala ya kusimama na watu.

Gideon Moi
Image: MAKTABA

Seneta wa Baringo Gideon Moi amepoteza kiti chake baada ya William Cheptumo kutangazwa mshindi katika kinyang'anyiro cha mwaka huu.

Cheptumo, ambaye aliwania kwa tiketi ya UDA, amekuwa mbunge wa Baringo Kaskazini kwa miaka 15.

Cheptumo alishinda kwa kura 141,777 huku Moi akiiuka wa pili kwa kura 71,408. Mgombea wa Party Party (TSP) Felix Chelaite alipata 3,261.

"Nawashukuru watu wangu kwa kunichagua kuwatumikia kwa miaka mitano ijayo kama Seneta wao" Cheptumo alisema.

Alizungumza alipokuwa akikabidhiwa cheti chake na afisa msimamizi wa kaunti ya Tume Huru ya Mipaka (IEBC) John Mwangi katika Shule ya Serikali ya Kenya (KSG) Baringo mnamo Ijumaa.

Hata hivyo Gideon ambaye ni mwanawe aliyekuwa rais marehemu Daniel Toroitich Arap Moi hakuhudhuria sherehe hiyo wala kujitokeza kukubali kushindwa.

Gideon ni mwana pekee wa marehemu Mzee Moi ambaye ameaminiwa kushikilia uongozi wa Baringo tangu kufariki kwa babake.

"Sasa familia ya Moi imekwisha, uhuru umefika" mkazi mmoja alisema. Hapo awali Gideon alikuwa na ugumu wa kueleza kwa nini anapata kura na kutoweka mara moja badala ya kusimama na watu.

Cheptumo hata hivyo aliahidi kuwaunganisha wakazi na viongozi wenzake waliochaguliwa katika kaunti ili kukabiliana na ukosefu wa usalama unaosababishwa na ujambazi na wizi wa mifugo.

Aliungwa mkono na mwakilishi wa wanawake wa kaunti hiyo Florence Jematia na Gavana mteule Benjamin Cheboi.

Jematia alisema “ni hadi tutakapomaliza ujambazi usiokoma ili tuanze maendeleo hapa Baringo"

Cheboi alipata kura 137,486 na kumng'oa gavana wa muhula mmoja Stanley Kiptis aliyepata kura 17, 646. Mbunge wa zamani wa Eldama-Ravine Moses Lessonet aliibuka wa pili kwa kupata kura 60,879.

Jematia pia alipata kura 144,039 na kumrejesha nyumbani mshindani wa sasa wa KANU Gladwel Cheruiyot aliyepata kura 40,302.

Mgombea huru Naomi Toronto, Rebecca Lomong wa Kenya United Party(KUP) na Sarah Chepkorir wa Chama Cha Mashinani(CCM) walipata 25,523, 25,129 na 4,605 ​​mtawalia.