logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Osoro - Haikuwa rahisi, mlinichagua bila kupokea hata bob kutoka kwangu, ahsante South Mugirango!

"Watu walikuwa wakipewa pesa na machifu waliokuwa wamevalia sare na kulindwa na Askari, Yaani Kila njama iliwekwa kwa meza.. lakini wapi,” Osoro alisherehekea.

image
na Davis Ojiambo

Uchaguzi13 August 2022 - 09:35

Muhtasari


  • • "Ahsante sana ndugu zangu, kura 25,000 si jambo dogo na hamkupata hata shilingi kutoka kwangu,” Osoro alisema.
Mbunge mteule wa South Mugirango, Slyvanus Osoro

Mbunge wa Mugirango ya Kusini Slyvanus Osoro amewashukuru wakaazi wa eneo bunge hilo lililopo kaunti ya Kisii kwa kumchagua kwa mara nyingine tena licha ya kile alikitaja kwamba majeshi mengi yalikuwa yamehamasishwa kusimama dhidi yake katika eneo bunge hilo.

Akitoa shukrani kupitia ukurasa wake wa Facebook baada ya kupokezwa cheti cha ushindi, Osoro ambaye ni mtetezi mkali wa sera za naibu rais William Ruto na ambaye alikuwa anawania kupitia chama cha UDA alisema kwamba washindani wake walikuwa wengi na walikuwa wameshirikiana na vyombo vya dola pamoja na Waziri Matiangi katika kuwezesha njama ya kumbwaga chini ila wananchi wakasimama tisti na kumchagua kwa wingi licha ya kutopata hata shilingi moja kutoka kwake, ikilingalishwa na washindani wake ambao alisema waliweka watu wa kuwarubuni wapiga kura na pesa katika vituo vya kupiga kura ili kutompigia Osoro.

“Hii nayo wasee haikuwa rahisi.Hata kama nimepiga majamaa kabisa na tofauti kubwa, tofauti na uchaguzi wa awali, hapa vita ilikuwa ni mimi dhidi ya watu wengi (majina), waliweka bajeti ya 500k katika KILA KITUO CHA KURA..watu walikuwa wakipewa pesa na machifu waliokuwa wamevalia sare na kulindwa na Askari, Yaani Kila njama iliwekwa kwa meza.. lakini wapi,” Osoro alisherehekea.

Osoro alisema wafuasi wake kumpigia kura elfu 25 si kitu rahisi pamoja na kumchagua diwani mmoja kwa UDA na wengine wawili kutoka vyama tanzu vya Kenya Kwanza si kitu rahisi.

“Lakini Mungu ni nani, watu walikula pesa, wakaingia kwa vituo vya kupiga kura na kumpigia chaguo lake ambaye ndio mimi. Ahsante sana ndugu zangu, kura 25,000 si jambo dogo na hamkupata hata shilingi kutoka kwangu,” Osoro alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved