Waziri wa Marekani Blinken amsifu Uhuru kwa juhudi zinazoendelea za kuleta amani

Blinken amempongeza Uhuru kwa juhudi zake za kuendeleza amani na usalama nchini Kenya.

Muhtasari

•Blinken alitoa wito kwa amani na uvumilivu wakati kujumlisha kwa kura za urais kumeshika kasi.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken akizungumza katika chumba cha taarifa cha Wizara ya Mambo ya Nje huko Washington, Marekani Januari 7, 2022.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken akizungumza katika chumba cha taarifa cha Wizara ya Mambo ya Nje huko Washington, Marekani Januari 7, 2022.
Image: REUTERS

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Anthony Blinken amempongeza Rais Uhuru Kenyatta kwa juhudi zake za kuendeleza amani na usalama nchini Kenya.

Blinken na Uhuru walijadili ziara yake ya kwanza ya hivi majuzi nchini Afrika Kusini, DRC na Rwanda na umuhimu wa uchaguzi wa Kenya kama mfano wa kuigwa kwa Afrika.

Alitoa wito kwa amani na uvumilivu wakati kujumlisha kwa kura za urais kumeshika kasi.

Ni tume la uchaguzi pekee linaloweza kutangaza mshindi baada ya kulinganisha na kuthibitisha matokeo kutoka kwa maeneo bunge.

Tume ya uchaguzi ina hadi siku saba baada ya siku ya uchaguzi kutangaza matokeo ya mwisho.

Ili kushinda kinyang'anyiro cha urais katika awamu ya kwanza, mgombea anahitaji:

zaidi ya nusu ya kura zote zilizopigwa kote nchiniangalau asilimia 25 ya kura zilizopigwa katika kaunti zisizopungua 24.Vinginevyo, zoezi la upigaji kura linakwenda kwa duru ya pili ambayo kwa mujibu wa sheria inapaswa kufanyika ifikapo tarehe 8 Septemba.