logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Uhuru Kenyatta asalia kimya baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu

Uhuru alikuwa anamuunga mkono aliyekuwa Raila Odinga kuchukua nafasi yake

image
na Davis Ojiambo

Uchaguzi17 August 2022 - 05:55

Muhtasari


  • • Alizungumza kwa ufupi na wanahabari Jumanne iliyopita baada ya kupiga kura.
Rais Uhuru Kenyatta

Ni wiki moja sasa tangu Wakenya walipomuona ama kumsikia Rais Uhuru Kenyatta.

Alizungumza kwa ufupi na wanahabari Jumanne iliyopita baada ya kupiga kura katika mji aliozaliwa nje kidogo ya mji mkuu, Nairobi.

Alikuwa anamuunga mkono aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kuchukua nafasi yake badala ya naibu wake, William Ruto, ambaye alitangazwa mshindi wa uchaguzi wa Agosti 9.

Wawili hao walipochukua madaraka mwaka wa 2013 walikuwa na uhusiano wa karibu, kila mara wakiitana “kaka”, wakipiga makofi hadharani baada ya kutaniana na wakati mwingine kuwa na mahusiano ya karibu sana.

Haijulikani kwanini walikosana, lakini uhusiano wao ulizidi kuwa mbaya na kuzorota kuelekea siku za kuelekea uchaguzi wa mwaka huu ambapo walirushiana maneno makali.

Licha ya Bw Kenyatta kutokuonekana hadharani, serikali yake ilitangaza siku ya Jumanne  kwamba mchakato wa kumpata Rais mpya bado unaendelea.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved