logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wacheni kuingilia siasa za Kenya,'Raila aambia mataifa ya kigeni

Raila alionyesha imani kwamba wana ushahidi wa kutosha

image

Uchaguzi22 August 2022 - 17:24

Muhtasari


  • Raila alionyesha imani kwamba wana ushahidi wa kutosha ambao unaona uamuzi wa Mahakama ya Juu kwa upande wao
Raila Odinga

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga amezitaka nchi za kigeni kukoma kuingilia siasa za Kenya.

Kiongozi huyo wa Azimio alizitaka nchi za kigeni kusubiri hukumu ya Mahakama ya Juu ambayo imepangwa kusikiliza na kuamua kesi iliyowasilishwa mbele yake.

Raila alikuwa akihutubia taifa katika KICC Jumatatu baada ya kuwasilisha ombi la uchaguzi wa urais alipotoa matamshi hayo.

"Ata marafiki wetu kutoka ng'ambo ambao wako hapa, tungependa kuwasihi wawe na subira. Wasijiingize katika mambo ya siasa ya kindani ya Kenya. Waache Wakenya wasuluhishe mambo yako kama wakenya."

Raila alionyesha imani kwamba wana ushahidi wa kutosha ambao unaona uamuzi wa Mahakama ya Juu kwa upande wao.

"Tuna uhakika ya kwamba tuko na ushahidi wa kutosha kuonesha kuwa sisi ndio tulishinda uchaguzi wa 2022,"Alizungumza Raila.

Siku ya Jumatatu, Balozi wa Uingereza nchini Kenya Jane Marriott alikariri kwamba Uingereza na yeye mwenyewe hawakuwa na mgombea aliyependekezwa zaidi katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9, mwaka huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved