logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakukuwa na viti vya MCA wa Azimio kwenye hafla ya Sakaja- Alai adai

Alai alisema walikuwa na mwaliko wa kuhudhuria hafla hiyo.

image
na Davis Ojiambo

Uchaguzi25 August 2022 - 09:21

Muhtasari


  • •Alai aliyechaguliwa kwa tikiti ya chama cha Orange Democratic Movement (ODM) alisema walikuwa wamealikwa kuhudhuria hafla hiyo.
Katika maandalizi ya kumuapisha gavana mteule wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja katika KICC mnamo Agosti 25, 2022.

Kundi la MCAs wa Azimio La Umoja- One Kenya walilazimika kuondoka kwenye hafla ya kuapishwa kwa Johnson Sakaja kama gavana wa nne wa kaunti ya Nairobi,mwanablogu Robert Alai amedai.

Akihutubia waandidhi wa habari, MCA huyo mteule wa Kileleshwa alisema walilazimika kuondoka kwenye hafla hiyo iliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Kenyatta (KICC) baada ya kubaini kuwa hakukuwa na viti vilivyotengewa MCAs wa Azimio.

Alai aliyechaguliwa kwa tikiti ya chama cha Orange Democratic Movement (ODM) alisema walikuwa na mwaliko wa kuhudhuria hafla hiyo.

"Tulialikwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Sakaja na hivyo tulihudhuria, lakini kulikosekana kwa viti vya kukalia, na haswa wale MCAs wa Azimio ndiyo walikosa viti, kwa hivyo, tulilazimika kuondoka," Alai alisema.

"Ni jambo la kushangaza sana kuapishwa kwa  Rais bila wabunge kupata viti. Tulikuwa zaidi ya 25. Kati ya MCAs 45 wa Azimio. Lakini tunataka kumhakikishia (Sakaja) kwamba kama MCAs wa Azimio, tuko tayari kumuunga mkono." Alai aliongeza.

Sakaja aliapishwa kama gavana wa nne wa Nairobi mwendo wa saa tano asubuhi ya Alhamisi katika ukumbi wa KICC. 

Hakimu Roselyn Aburili ndiye aliyesimamia hafla hiyo.

Mamia ya wageni waalikwa wakiwemo wanasiasa mashuhuri walishuhudia kuapishwa kwa Sakaja moja kwa moja. 

Rais mteule William Ruto ni miongoni mwa wageni waliokuwa wamehudhuria.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved