logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo achukuwa karatasi za uteuzi kuania wadhifa wa spika wa Seneti na bunge

Aliyekuwa seneta maalum Isaac Mwaura, pia amechukua stakabadhi za uteuzi wa spika wa seneti.

image
na Davis Ojiambo

Uchaguzi06 September 2022 - 14:47

Muhtasari


  • • Makamu huyo wa zamani wa rais pia alikuwa amechukua stakabadhi za kutafuta wadhifa wa spika wa Bunge la Kitaifa na sasa tena ameweka mtego katika seneti.
  • • Wengine ambao wamechukua karatasi hizo kufikia sasa ni Isaac Aluoch, Jared Oundo, George Bush, Dkt Rodgers Manana, Beatrice Kinyua, Dorothy Kemunto na Jecinta Lesiangiki.
  •  

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka ni miongoni mwa watu 15 ambao wamechukua karatasi za kuteuliwa kuwa spika wa Seneti.

Makamu huyo wa zamani wa rais pia alikuwa amechukua stakabadhi za kutafuta wadhifa wa spika wa Bunge la Kitaifa na sasa tena ameweka mtego katika seneti.

Washirika wa Rais mteule William Ruto, aliyekuwa Gavana wa Kilifi Amason Kingi, na aliyekuwa mgombeaji wa ugavana wa Mombasa Hassan Omar pia walikuwa wamechukuwa stakabadhi hizo kufikia saa tisa kasorobo jioni Jumanne.

Aliyekuwa seneta maalum Isaac Mwaura, ambaye alihudumu katika jopo la spika kwenye bunge lililopita pia amechukua stakabadhi za uteuzi wa spika wa seneti.

Katika Seneti, Kalonzo alikuwa miongoni mwa watu 15 ambao walikuwa wamechukua karatasi za uteuzi kwa nafasi ya spika na wawili kwa nafasi ya naibu spika.

Watu wengine ambao wamechukua karatasi hizo kufikia sasa ni Isaac Aluoch, Jared Oundo, George Bush, Dkt Rodgers Manana, Beatrice Kinyua, Dorothy Kemunto na Jecinta Lesiangiki.

Josephat Mutua, Mohamud Halake, Michael Gichuri na Joshua Boit pia walichukuwa karatasi za uteuzi katika Bunge.

Kwa nafasi ya naibu spika, Maseneta wateule Karungo wa Thangwa (Kiambu) na Kathuri Murungi (Meru) walikuwa wamechukua karatasi.

Hata hivyo, kinyang'anyiro hicho kitajulikana baada ya kujua ni nani kati yao atakuwa amerudisha karatasi kufikia Jumatano, saa nane alasiri.

Karatasi za uteuzi zitakazorejeshwa pia zitachunguzwa ili kuhakikisha kuwa wagombeaji wanaafikia vigezo vya sheria.

Maseneta wateule watamchagua spika mara baada ya kuapishwa siku ya Alhamisi.

Spika mpya atamrithi Ken Lusaka ambaye alichaguliwa kuwa gavana wa Bungoma kwenye Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved