Hali ya mtafaruku imezuka tena katika ukumbi wa Bomas of Kenya na kusimamisha zoezi linaloendelea la uhakiki wa kura za urais.
Mawakala wanaoshirikiana na muungano wa Azimio walikuwa wakidai kuwa kuna kasoro katika zoezi la uhakiki.
Baadhi yao walidai kuwa baadhi ya maafisa wa IEBC walikuwa wakishirikiana na wapinzani wao kubadilisha matokeo na kunyakua fomu 34 A.
Mara moja, ajenti mkuu wa Raila Saitabao Ole Kanchory alitembea hadi jukwaa la VIP ambapo mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati na timu yake huketi, akanyakua kipaza sauti na kusema:
"Nataka kuwaambia Wakenya kwamba Bomas ni eneo la uhalifu."
Hadi wakati wa ripoti hii, zoezi la uhakiki wa kura lilikuwa limesimama.