Uchawi?‘Niliambiwa nitayarishe uji wageni wanakuja,Kumbe ni Nyoka aliyefaa kunywa uji!’

black snake
black snake
Zama za kale kabla ya mtu kuoa au kuolewa ilihitajika  uchunguzi kufanywa ili kuwafahamu watu wa boma ambako  angelikwenda kuoa au kuolewa mtu ili asijipate katika masaibu ya kuolewa katika boma ‘ baya’ kama walivyosema . ‘ Boma baya’ katika muktadha huo lilikuwa la watu waliodaiwakuwa wachawi au warogi ukitumia  maneno yanayofahamika na wengi . Lakini ilionekana kama  visa tu vya kutisha  na wengi walivichukulia kwa mzaha hadi wakati huu  ambapo  Alice  Ochola ameelezea masaibu yaliomfika alikoolewa kwa miezi mwili huko Nyakach . Baada ya kukutana na mwanamme waliyependana naye na kufanya uchumba kwa muda mrefu hapa Nairobi ,ilipigwa karamu ya wao kwenda nyakach ili kuweza kufahamishana  na familia yake kuhusu uamuzi wao kutaka kufunga ndoa .

Kwa sababu ya kipato chao kidogo ndoa yao haikuwa ya bonge la sherehe na mbwembwe ila baada ya wazazi wa pande zote kujulishwa na kutambulishana ,wapendanao walianza kuishi pamoja  kama mke na mume .Kila kitu kikawa sawa kwa mwezi mmoja lakini katika moyo wake kuna uzito ambao ulimjia Alice akiwa katika boma la kina mumewe . Alishangaa mbona wanakijiji walimuangalia kwa huruma ni kana kwamba kuna jambo walilotaka kumwambia .Kila alipokwenda mtoni kuteka maji ,angekutana na wanawake wa kijiji wakiendelea pia na shughuli zake na baada ya kumsalimu wangemuuliza iwapo aliolewakatika boma Fulani .Alipojibu ndiye mke mpya katika boma hilo ,wengi walimuepuka na kuendelea na shughuli zao na alishangaa mbona .Hata hivyo kwa sababu ya  ustaarabu alifikiri haingekuwa jambo la buara kumuuliza mume wake mambo kama hayo  Ila hakujua yalimgonja !

‘USIWAHI KUOLEWA AU KUOA KATIKA BOMA LA WATU USIOWAJUA VIZURI.FANYA UCHUNGUZI USIJE UKAOLEWA KATIKA FAMILIA YA WEZI,WACHAWI NA KADHALIKA’  amesema Alice

Siku moja asubuhi mama mkwe alimwita  Alice   na kumfahamisha kwamba kuna wageni ambao watakuja jioni hiyo kwa hivyo afanye matayarisho la kufanya usafi na kufagia visehemu vilivyodondokwa na matawi na kasha atayarishe uji mzuri wa wimbi . Duh! Ilionekana kazi rahisi mtoto wa wenyewe akajua muda mfupi ujao atamaliza shughuli hiyo na awangoje wageni . Ilipotimu majira ya  jioni , gsa likikaribia , Alice akaketi nje ya chumba chake akingoja basi wageni waje na alijua wataingia katika nyumba ya mama mkwe wake . Muda mfupi baadaye ,mama mkwe alimuambia alete uji ambao aliutayarisha auweke nje  hapo karibu na nyumba yake kasha akae kando .Mgeni alikuwa njiani anakaribia kuja . Akashangaa mbona tena mgeni apewe uji akiwa nje ? Mbona tena wenyeji watangoja katika vibaraza vya nyumba zao wakimuangalia mgeni akinywa uji? Lakini muda haukumpa dakika za kuweza kupata majibu .

‘SIKUTAKA KUJUA KAMA NILIMPENDA MUME WANGU.THE FACT  THAT KWAO KULIKUWA NA NYOKA NILISALIMU AMRI’ Alice anasema

Pembeni Alice alimsikia mama mkwe akijawa na jazba ya  kiasili akiimba wimbo uliosikiza kama wa kitamadauni na kilichokuja karibu na sehemu ambapo uji uliwekwa ni Joka kubwa jeusi ambalo lilimfanya kaishiwa nguvu miguuni! Asijue la kufanya,maskini mtoto wa wenyewe alizirai. Wakati ‘mgeni’ alipokuwa akinywa uji, Alice alikuwa amepoteza fahamu !

‘SIKU HIZI WATU HUKUTANA KATIKA MIJI NA WANAANZA UHUSIANO BILA KUJALI KUHUSU HALI YA WENZAO WANAKOTOKA,FANYENI UCHUNGUZI KWANZA,HUFAI KUWA NA HARAKA KUINGIA KATIKA NDOA’ Alice anashauri

Baadaye usiku huo ,akiwa sasa amepata fahamu ,mume wake walimweleza kuhusu  ‘utamaduni wao’ na Yule’mgeni’ aliyekuwa kunywa  uji . Mumewe alimuambia Yule nyoka yupo kika kizazi chao na kwa hivyo wanamlinda nay eye pia anawalinda kama familia na ukoo . Kwa ufupi Alice  aligundua familia ile ilikuwa ya wachawi wa kuroga kumtumia Yule nyoka .Mwanzoni ilionekana kama ndoto lakini  mtoto wa wenyewe keshoye , hakuweza kufikiria hata kufungasha chochote chake, alitoroka alivyokuwa nakurejea kwao.Ndoa yake ilifikika tamati papo hapo na hajawahi kuangalia nyuma .Umeshawahi kuyasikia kama haya?