Ugonjwa wa kansa  ndio uliosababisha kifo cha mbunge  wa Msambweni  Suleiman Dori

 Mbunge wa Msambweni Ramadhan Suleiman Dori  amezikwa leo  nyumbani kwake katika  kijiji cha Gazi ,eneo bunge la  Msambweni huko Kwale .

Chama cha ODM kilichompa tiketi ya kwenda bungeni kimesema mbunge huyo aliaga dunia kwa sababu ya kansa ." Tumehuzunishwa na kifo cha mwanachama  wetu na  mbunge  wa Msambweni Suleiman Dori  mapema leo . Kansa  ,imemchukua tena kiongozi aliyejitolea wa Kenya . kwa watu wa msambweni, kaunti ya Kwale na eneo zima la Pwani  poleni sana,"  Chama hicho kimeandika katika ukurasa wake wa Twitter.

Dori aliaga dunia katika hospitali ya Aga Khan  ambako alilazwa katia kitengo cha ICU. Mkurugenzi wa  Mamlaka ya ustawi  Pwani   Mshenga Rugha alialisema Dori alianza kuugua Jumapili na kukimbizwa katika hospitali hiyo. Mbunge huyo mwenye umri wa miaka 42  alikuwa akihudumia muhula wake wa pili kama mbunge wa eneo bunge hilo kwa tiketi ya chama cha ODM .

Kiongozi wa ODM Raila Odinga   na rais  Uhuru kenyatta pia walituma risala zao za rambirambi kwa familia ya Dori .