Rais Uhuru Kenyatta amehamia jumba la Harambee baada ya ikulu kufungwa wafanyikazi wanne walipopatikana na virusi vya corona .
Rais Kenyata amesema hajapatikana na virusi hivyo na amekuwa akifanya kaz katika jumba la Harambee iliyotajwa kuwa salama .wafanyikazi wake pia wamehamia jengo hilo naye .
Rais Kenyatta amekuwa akifanyia kazi Ikulu ya Nairobi hadi visa vya corona vilivporipotiwa Juni tarehe 15 katika makao hayo yake .mikutano yake yote sasa imekuwa ikifanyika Harambee .
Kabla ya visa hivyo vya corona kuripotiwa Ikulu rais alikuwa akiandaa mikutano yake yote ikiwemo na wabunge na baadhi ya wanasiasa katika Ikulu .