Uhuru aifurusha bodi ya Huduma za Feri

Rais Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi aliwapiga kalamu wanachama wote wa bodi ya huduma za feri nchini kutokana na mkasa uliosababisha vifo vya Mariam Kighenda na mwanawe Amanda katika feri ya Likoni.

Kwenye gazeti rasmi la serikali la tahere 16 Okotoba, Uhuru alifutulia mbali uteuzi wa Dan Mwazo kama mwenyekiti wa bodi hiyo na wanachama Daula Omar, Naima Amir, Philip Ndolo na Rosina.

Notisi hiyo kutoka ikulu ilisema:

“IN EXERCISE of the powers conferred by section 7 (3) of the State Corporations Act, I, Uhuru Kenyatta, President and Commanderin-Chief of the Defence Forces of the Republic of Kenya, revokes the appointments of Dan Mwazo, Daula Omar, Naima Amir, Philip Ndolo, Rosina Nasigha Mruttu, as Non-Executive Chairperson and members of the Kenya Ferry Services Limited, with effect from the 16th October, 2019,”

Kulingana na ripoti za daktari, Mariam na Amanda walifariki kutokana na kukosa hewa ya oxijeni baada ya kuzama majini.

Miili ya wawili hao iliopolewa kwenye bahari siku 13 baaada ya ajali hiyo.