Uhuru amhongera waziri mkuu ,mpya wa Japan Suga na kumuaga Shinzo Abe

Suga
Suga
Rais Uhuru Kenyatta amemhongera  waziri mkuu  mpya wa Japan  Yoshihide Suga  kufuatia kuchaguliwa kwake kama kiongozi mpya wa taifa hilo . Suga anaichukua nafasi ya Shinzo Abe ambaye  anang’atuka madarakani kwa sababu ya kudhoofika  kwa hali yake ya afya .

Katika ujumbe wake   kwa Suga rais Uhuru Kenyatta amemtakia kila la heri na  kumuahidi kujitolea kwa Kenya kuendeleza uhusiano wa muda mrefu katika ya Kenya na Japan .

Amesema anatarajia  kujenga uhusiano wa karibu Zaidi na utawala wake  na kuzidisha biashara kati ya Kenya na taifa hilo la bara Asia .

Wakati huo huo rais Kenyatta pia amemuaga waziri mkuu anayeondoka Shinzo Abe  akimshukuru kwa kuwa kiongozi aliyetegemewa kuendeleza uhusiano kati ya Kenya na Japan .

Amesema kupitia Abe Kenya ilipata ,msaada wa kifedha kuweza kufanikisha miradi kadhaa ya miundo msingi  katika sekta za ujenzi wa barabara ,kawi  na eneo maalum la EPZ huko dogo Kundu  katika kaunti ya Mombasa