Watoto wawili wasichana ambao ni dada walio na umri wa miaka sita na tisa walibakwa jumatano usiku na kisha kuuawa katika eneo la kaunti ya Kisii .
Ripoti zaarifu kuwa watoto hao walikuwa nyumbani pekee yao wakati wa tukio hilo kwa sababu mama yao alikuwa meenda sokoni .
Kamanda wa polisi wa kaunti ya Kisii Martin Kibet amesema huenda watoto hao waliuawa baada ya kuwatambua waliotekeleza unyama huo . Visa vya ubakaji na wakati mwingine mauaji ya watoto vimekuwa vikiripotiwa kwa wingi katika sehemu mbali mbali za taifa .