Daddy Owen ni mwanamziki wa nyimbo za injili ambaye alijifunga kibwebwe na kutia bidii sana ili kufaulu maishani kwani nafikiri alisadiki methali,mtaka cha mvunguni,sharti ainame.
Hata ikiwa Daddy Owen alikuwa na ndugu ambaye alikuwa ashafanya vyema kimuziki,Bwana Rufftone, ni wazi kuwa hakukata tamaa bali alizidi kutia bidii na kumcha Mungu.
Aisee mtegemea cha nduguye hufa maskini.
“Daddy Owen alikuwa anatesa industry vizuuuuri… alafu akaoa. Smh,” Nixon aliandika.
''Oneni huyu sasa na kiherehere….hawa ndio wajuaji wa Nairobi ama? 🤣🤣🤣 anyway .. the Bible talks about seasons.. thrs time for everything my brother.''Daddy Owen alisema.
Owen Mwatia (Daddy Owen) alifunga pingu za maisha na mpenzi wake Farida Wambui mwaka wa 2016 na wamebarikiwa na mtoto mmoja wa kiume.
Wapenzi hawa walikutana kwenye mkahawa wa Java, wakabadilisha namba na wakaendelea na uhusiano wao kwa miaka minne kabla ya kufunga pingu za maisha.Amini usiamini, hata ikiwa Daddy Owen ni 'Celebrity' ndoa yake na mke wake haijawahi kuwa na vioja .