Ulikuwa umeenda kusukwa nywele zako? Akothee hamwamini Rue Baby

Akothee alikabiliana na binti yake, Rue Baby, baada ya Rue Baby kurudi nyumbani baada ya saa alizoelekezwa kupita.

Katika video ya Instagram, Akothee alimuliza,

Ulifika nyumbani saa ngapi jana? Hukujua kwamba nilikuwa hapa? Nilikuwa Nairobi? Nilikusubiri hadi saa 11:00 za usiku.

Rue Baby alijibu kwa udhaifu,

Nilienda kusukwa nywele zangu.

Akothee hakukubaliana na sababu ile na kumjibu,

Usiku wa manane?  Jiji la Nairobi? Ulikuwa umeenda kusukwa nywele zako?

Rue aliendelea na kusema kuwa kulikuwa na mstari mrefu ndio maana alichelewa.

Akothee aliendelea kusema

 Endelea kusukwa nywele zako, hadi tumbo yako iwe kubwa. Kisha utakuja kujua kuwa unasukwa nywele zako. Suka nywele zako tangu saa 5 asubuhi

Soma mengi