'Ulinzi bora wa mwanamke nikuwa na ujasiri,'Mkewe Alikiba asema

Hivi karibuni mkewe msanii wa nyimbo za bongo Alikima Amina Khalef amekuwa akiwatia moyo mashabiki wake kwenye mitandao ya kijamii.

Kupitia mitandao yake ya kijamii alipost picha akiwa amevalia rinda nyeusi, na kuwaambia wanawake wajioe moyo licha ya yale yote wanapitia.

"The best protection any woman can have is courage😊."Aliandika Amina.

Akisherehekea sikuku ya Eid alipost picha yake na mwanawe Keyaan Ali, huku akiwatakia watu wote uvumilivu na hata kuwa na utu wakati huo.

"May you be blessed with kindness, patience and love. Eid Mubarak to all❤️."

Kabla ya hayo Amina amekuwa akiposti jumbe za kushangaza, hii ni baada ya mwanahabari wa Tanzania Diva The Bause kusema kuwa alikuwa mchumba wa Alikiba akiwa bado katika ndoa na Amina.

Kupitia mitandao  ya kijamii Amina alipost wanaume ambao wamekuwa wametanda sana wakiwa wamebeba jeneza huku wakisakata nyimbo tofauti baada ya hapo jicho pevu limekuwa likiwamulika Alikiba na mkewe baada ya kuachana.

Katika mitandao hiyo hiyo, alipost picha inayosoma kuwa baada ya mtu kupitia shida na hata magumu ya maisha mwisho atapata ushindi.