Yote yalianza wakati walipokutana na katika eneo moja la Burudani katika huko Bamburi Mombasa na wakabadilishana nambari za simu . wiki kadhaa badaye walikutana tena kwa chakula cha jioni katika mkahawa mmoja, Huku Chule akikosa kufahamu kwamba alikuwa akitembea na mtoto wa shule . Mambo yake yalimwendea vibaya wakati mmoja wa walimu wa msichana huyo alipowaona katika mkahawa huo na kumwita ili kumuuliza mbona alikuwa anatembea na mwanafunzi wake .
Chule alishangaa kwa sababu mtoto huyo wa skuli alikuwa amemhakikishia kwamba ametimu umri wa kuwa mtu mzima n ahata akamuonyesha kitambulisho . Baadaye walipoendelea kuonana , kumbe mwalimu alikuwa amempigia simu mamake msichana huyo na kumshauri aripoti kwa polisi ili Chule akamatwe kwa ‘kumharibu’ msichana wa shule .
Chule alikuwa aktika utaratibu wa kujua ukweli iwapo msichana yule alikuwa na umri wa miaka 23 kama alivyodaiwa wakati maafisa wa DCI pamoja na Chifu walipomkujia katika duka lake ka elektroniki mjini Mombasa na kumweka korokoroni kwa ‘kutembea’ na msichana wa shule .Ufichuzi baadaye umebaini kwamba msichana yule alikuwa akitembea na kitambulisho cha dadake na kwa sababu wanafanana hakuna aliyegundua kwamba mtoto wa shuke alikuwa akijifanya kuwa dadake mkubwa .
Chule ameachiliwa huru kwa dhamana lakini kesi dhidi yak inaendelea hasa wakati huu ambapo mashirika mengi ya serikali yamejitolea kupambana na wanaume wanaofanya mapenzi na vitendo vya utu uzima na wasichana wadogo . Ameendelea kujitetea kwamba hakujua umri wa msichana huyo wa shule ,lakini polisi na mahakama haijamuamini ingawaje kwa bahati nzuri amefaulu kuwashawishi wazazi kwa msichana yule kwamba hakuwa na nia ya kumharibu binti yao hasa baada ya kudanganywa na kitambusho cha dadake mkubwa alichokuwa akikitumia kama chake .