Mahakama ya ajira na Leba imetupilia mbali uamuzi wa waziri wa elimu George Magoha kufutilia mbali uteuzi wa Stephen Kiama kama Naibu Chansela mkuu wa Chuo Kikuu cha Nairobi . Jaji Maureen Onyango pia amesitisha kuteuliwa kwa Profesa Issac Mbeche kama kaimu naibu chansela mkuu wa chuo hicho . Agizo hilo litasalia kuwepo hadi februari tarehe tani wakati kesi hiyo itakaposikizwa .
Katika notisi aliyotuma siku ya jumapili waziri Magoha alisema mshikilizi wa kudumu wa wadhifa huo atateuliwa baada ya mashauriano. Lakini aliongeza kwamba Kiama angeendelea kuhudumu katika wadhifa wake wa hapo awali kama naibu chansela anayesimamia wafanyikazi na utawala .
Tangazo hilo lilitolewa baada ya Kiama kutuma mwaliko kwa umma kwa hafla ya kukabidhiwa rasmi hatamu kama VC januari tarehe 21 . Badaye mwaliko huo ulifutwa baada ya kuzuka vuta ni kuvute kuhusiana na usimamizi wa Chuo . Kiama ametuma taarifa akisema hatosalimisha majukumu yake kama mkuu wa taasisi hiyo licha ya agizo la Magoha