Akizungumza na wanahabari kutoka hospitali ymoja ya kibinafsi anakouguza jeraha ya risasi miguuni, mwanawe marehemu Eric Wafula Barasa amesema babake alipigwa risasi mwendo wa saa sita usiku mda mfupi tu baada ya kuwasili kutoka sokoni anakofanyia biashara.
Amesema juhudi zao za kujinasua hazikufua dafu huku dadake zake wawili wakinajisiwa na genge hilo kwa takribani masaa mawili huku maafisa wa polisi wa kambi ya chebukwabi wakidaiwa kuchelewa kuwasili mahali pa tukio hilo.
Hata hivyo, wanasiasa wa eneo hilo wakiiongozwa na Didmus Baraza na Aggrey Mulongo wameshtumu tukio hilo na kuomba kamishna wa kaunti ya Bungoma Joshua Chepchieuhang kuhrakisha uchunguzi la sivyo waandae maandamano dhidi ya vitengo vya usalama vya eneo hilo.
Hakuna mshukiwa yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.