Unyama wa polisi! Mwanamke apigania uhai wake baada ya gari lake kufyatuliwa marisasi na polisi

Mwanamke anaendelea kupigania uhai wake baada ya gari lake kufyatuliwa marisasi katika maeneo ya Emali/Loitoktok kwa kile maafisa wa polisi wanasema kuwa alikataa kusimamisha gari baada ya maafisa hao kumwambia.

Kulingana na polisi hao, mwanamke huyo alikuwa anaendesha gari hilo akielekea Loitoktok alipoamua kukiuka amri zao.

Mkuu wa polisi kaunti ya Kajiado Beatrice Gachago amesema maafisa wa usalama eneo hilo walikuwa wamepokea taarifa kuhusiana na gari lililokuwa limeibwa. Gachago ameongezea kuwa gari alilokuwa analiendesha mwanamke huyo lilikuwa linafanana na lile walililokuwa wanatafuta maafisa hao.

 “The officers stopped the woman as she approached a police roadblock in the Mashuuru Sub-County jurisdiction but refused,” alisema Gachago.

Walioshuhudia kisa hicho wanasema mwanamke huyo alikuwa analiendesha gari hilo akielekea eneo la kizuizi na alipoambiwa asimame akakataa, jambo lililowafanya polisi kumfyatulia risasi.

Kwa sasa mwathiriwa amelazwa katika hospitali ya Makindu akiuguza majera ya risasi tano, taarifa ambazo zimethibitishwa na mkuu wa afya katika hospitali hiyo ya Makindu David Kasanga.

 "There is a consultant surgeon who is trying to save her life since she has lost a lot of blood following these injuries. He is currently assessing the damage on the stomach, to repair that first to stop more loss of blood,” amesema Kasanga.