Mwanamme mmoja huko Kangundo katika kaunti ya machakos amekamatwa na polisi baada ya kufanya kitendo cha ngono na mbwa wa familia yao hadi kumwua .Chifu wa eneo la Isinga Bethuel Kingele amesema Boniface Wambua mwenye umri wa makamo alipatikana na mamake akifanya kitendo hicho . Kingele pia amesema mipira ya kondomu iliyotumiwa ilipatikana katika eneo la kisa hicho . Hata hivyo inaripotiwa kuwa jamaa huyo hivi karibuni amekuwa akifanya vitendo visivyo vya kawaida na huenda anashiwishiwa na dawa za kulevya anazotumia .
Mamake mshukiwa amesema alishuku kuliwa na tatizo wakati aliposkia mbwa huyo akipiga kamsa kwa muda mrefu .Mshukiwa huyo amezuiliwa katika kituo cha polisi cha Kangundo na atafikishwa kortini siku ya alhamisi . Polisi walimlazimisha mshukiwa kumbemba mbwa huyo kama ushahidi