Wanawake hao walikuwa wanataka mjane Sylvia kunyimwa madaraka ya kusimamia mali hiyo peke yake. Jonathan alikuwa mwanawe Rais mstaafu Daniel Moi.
Jaji Aggrey Muchelule aliamuru watoto hao 6 kutajwa kama wanufaika wa mali hiyo baada ya makubaliano baina ya pande zote mbili katika kesi hiyo.
Jaji huyo pia aliagiza wahusika kukusanya na kuleta mahakamani orodha ya mali hiyo kwa wiki mbili zijazo.
Joshua Mutai pia aliruhusiwa kushiriki katika kesi hiyo kwa niaba ya wadai. Idhini hiyo ilitokea baada ya wanawake hao wawili pamoja na mutai kuwasilisha pingamizi.
Beatrice na Faith walisema kuwa walifunga ndoa kihalali na Jonathan Moi. Walimshtaki Sylvia kwa kudai kuwa ndiye mjane pekee wa Jonathan na kuenda kortini kutafuta barua za utawala huku akiwatenga.
Sylvia alikuwa ameiomba korti kumruhusu kusimamia mali hiyo kwa madhumuni ya kulipa kodi.
Kesi hiyo itatajwa mnano Desemba 11.