Katibu wa utawala wa Afya Dr Mercy Mwangangi amesema ingawaje Nairobi na Mombasa zote zimeorodheshwa kama kaunti hatari kwa ajili ya idadi ya juu ya visa vya COVID 19, Mombasa ina visa vya juu vya maambukizi ikilinganishwa na Nairobi.
Nairobi inaongoza kwa visa 2,428 ikifutwa na Mombasa kwa visa 1,304. Kaunti za Busia na Kajiado ambazo zina visa vingi kutokana na uwepo wa madereva kutoka nchi jirani zina visa 361 na 179 mtawalia.
Kulingana na Mwangangi, licha ya Mombasa kuwa ya pili kwa idadi ya visa ina uwezo mkubwa wa maambukizi kwa asilimia 107.9 ikifuatwa na Nairobi kwa asilimia 55.2 kwa kila idadi ya watu laki moja.
Mwangangi amesema Kenya ndio nchi pekee inayotumia utaratibu wa kuwapa utunzi na matibabu wagonjwa wa corona wakiwa nyumbani kama njia moja ya kupambana na virusi hivyo.