Vanessa Mdee aachana na mpenzi wake Juma Jux

Mwanamziki Vanessa Mdee ametangaza rasmi kwamba ameachana na aliyekua mpenzi wake Juma Jux. Wawili hao kutokea nchi jirani ya Tanzania wamekua kwenye mahusiano kwa mda mrefu.

Kwenye mtandao wake wa Instagram, Vanessa Mdee aliulizwa na shabiki mmoja kama ameachana na Juma.

Mdee alijibu "Ndio, lakini sisi ni marafiki wazuri na daima, tutakua familia"

Siku kadhaa zilizopita, dada ya Vanessa kwa jina Mimi Mars aliweka wazi kwamba wawili hao walikua wameachana, japokua Vanessa na Juma walikua wamekataa kuongea kuhusu jambo hilo.

Sasa ni wazi kwamba Vanessa hayupo katika mahusiano.