(+ Video) Diamond Platnumz ampiga Ali Kiba chambo kali, BABA LAO

Diamond-Platnumz-Baba-Lao-700x393
Diamond-Platnumz-Baba-Lao-700x393
Staa na nyota mkubwa wa muziki Afrika Diamond Platnumz amedondosha mkwaju mpya Baba Lao.

Aidha katika mistari ya Diamond Platnumz, mistari ipo inayoonekana kumlenga Ali Kiba kuhusu bifu yao iliyotamba katika mitandao ya kijamii.

"Ame-force bifu...eeh tumemkwepa...anabaki masononeko"

Huu ni mstari ambao upo kwenye ngoma hiyo.

Midundo ya muziki huu inadaiwa kuwa sawa na wimbo wa Soapy wake Naira Marley.

Kufanana kwa ngoma hizi mbili zimeifanya ngoma ya Diamond Platnumz kupata nafasi kubwa katika soko la muziki Nigeria.

Ngoma yake Diamond ina masaa kumi na 16 tangu iachiliwe kwenye mtandao wa YouTube.

Kati ya mistari kwenye Baba Lao, staa huyu anasifia lebo ya Wasafi na kutoa michambo inayoonekana kumlenga Kiba.

(+ Picha) Levis Saoli atua Citizen TV, alichokisema Nimrod Taabu,Joe Ageyo

Je,unadhani Mondi katoka na midundo ya Soapy? Dondosha maoni yako hapo chini?