(+Video yavuja) Mariam Kighenda akicheza Kainama ya Harmonize kabla ajali Likoni Feri

Mariam-and-Amanda-696x418
Mariam-and-Amanda-696x418
Video ya marehemu Mariam Kighenda akila bata na kupiga densi imevuja katika mitandao ya kijamii.

Kipande hiki cha video kinaaminika kuwa kilichukuliwa siku chache baada ya Mariam Kighenda kuhusika katika ajali mbaya feri ya Likoni.

Katika video hii, nyimbo ya Harmonize Kainama inasikika ikipiga chini kwa chini.

Miili ya wawili hawa ilitolewa Bahari Hindi siku 13 baadaye.

Hii hapa video;

https://www.instagram.com/p/B3lbb2eF3DS/

Uchunguzi wa kina unafanyika kubaini chanzo cha ajali hii.

Miili hii imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha Jocham, Mombasa.

Ulegevu wa serikali wa kutatua majanga yanayotendeka baharini sasa yameonekana waziwazi.

Nyufa hizi zimejitokeza waziwazi katika operesheni hiiya siku 13 za kuitoa miili na gari la Mariam Kighenda.

Gari la wawili hawa ilizama majini Sep 30 na imechukua majuma mawili operesheni kumalizika.

Hali ya kupuuza mikakati iliyopo na sheria za usalama katika shirika la feri zimeonekana dhaifu sana.

Inaaminika kuwa presha kubwa ya wakenya ilikuwa kwa jeshi la wanamaji kuutoa mwili huo kabla ya Oktoba 20 siku ya Mashujaa.

Hafla hii itakuwa karibu na eneo hilo la tukio.

Kenya imefanya shughuli hiyo baada ya kutafuta msaada wa wanamaji kutoka Afrika Kusini.