Viongozi wa Ukambani waapa kupinga mswada wa ugavi wa fedha katika bunge la Seneti

mutula-696x464
mutula-696x464
Maseneta kutoka Ukambani sasa wameapa kupinga vikali mswada wa ugavi wa fedha utakaorudishwa ndani ya bunge la seneti wiki hili kwa mara ya saba mfululizo.

Wakiongozwa na seneta wa Makueni Mutula Kilonzo ,viongozi hao sasa wamekashifu hatua ya vyama vya kisiasa nchini kuendelea kuwashinikiza maseneta kuunga mkono mswada ambao unanuiya kuhujumu mfumo wa ugatuzi nchini.

Jumanne maseneta wanatarajiwa kurejelea vikao vyao vya kawaida na kujadili mswada huo katika hatua ambayo imenasemekana kuewa huenda ikaashiria msimamo wa kisiasa nchini.

Maseneta hao ambao wametoka madeneo tofauti ya Mashhariki mwa Kenya,wamemkashifu kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka kwa kujaribu kuwashurutisha kuunga mkono mswada huo.

Kwa kauli moja sasa wamesema kuwa hawatashinikizwa kufanya uamuzi wao kivyovyote vile.

Maseneta sasa watalazimika kujadili mapendekezo yaliyoewasilishswa na seneta wa Nairobi Johnson Sakaja ambayo yanapania kutafuta suluhisho kwa mgogoro unaoenfdelea wa ugavi wa fedha .