Ekirapa alisema kuwa alitaka kuwa daktari ilhali hakuweza kwa maana hakupita sana.
Huku akizungumzia uhusiano wake wa awali alisema haya,
"Niliachwa na aliyekuwa mpenzi wangu mara tatu katika miaka nne ya uchumba, aliniambia kuwa alikuwa anataka kuenda kuomba ili kuuliza Mungu kama mimi kweli ni wake
mara ya kwanza kuniacha nilikuwa hospitali baada ya kupata ajali, aliniambia kuwa hana amani kutuhusu
Baada ya hapo nilingoja mwaka mmoja, lakini sikufahamu kuwa ana mpenzi mwingine,baada ya kungoja alirejea na tukaanza uhusiano tena
Alienda tena na kurudi baada ya mwaka mmoja alienda na kisha akarudi na kusema ana hakika kuwa mimi ni mpenzi wake
Tulienda kwa wazazi miezi nne kabla ya harusi yetu alienda tena." Alieleza Grace.
Baada ya uhusiano huo kukamilika Grace alipata mwanamume mwingine na kubali uhusiano wake kwa maana alikuwa amekata tamaa.
Pia alisema kuwa mwanamume huyo alilipa mahari ilhali alimuacha na kumuumiza moyo.
Kwa mengi zaidi tembelea youtube ya Radiojambo kwa mengi zaidi.