Baba yangu aliamini kuwa ninataka kuwa mchekeshaji aliponiona kwa gazeti-Mulamwah

Muhtasari
  • Mwaka jana Mulamwah alivuma kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutoka kwenye tasnia ya burudani

Katika kitengo cha ilikuaje tulikuwa naye mchekeshaji David Oyando almaarufu Kendrick Mulamwah ambaye aliweka mambo kadha wa kadha wazi.

Mwaka jana Mulamwah alivuma kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutoka kwenye tasnia ya burudani.

"Nilianza kukajeliwa kwenye mitandao ya kijamii ya twitter ambapo wanamitandao walikuwa wanakejeli kila kitu kunihusu

 
 
 

Ukianza kukejeliwa kwenye mitandao ya twitter hapo ni kama umeingia jehenamu, baada ya kejeli hizo nilipatwa na msongo wa mawazo," Alieleza Mulamwah.

Huku akizungumza kazi yake ambayo alisome chuo kikuu alisema,

"Nilisomea kazi ya uuguzi, mimi ni muuguzi baada ya kumaliza masomo yangu niliendaa katika hospitali kuu ya Kenyatta kwa mafunzo

Baba yangu hakupendezwa na hatua yangu ya kuwa mchekeshaji, wakati mmoja aliamka na kuniona kwa gazetti, na nikaanza kuanya mabadiliko nyumbani, hapo ndipo aliamini kwamba napenda kazi ya uchekeshaji

Aliniambia kama nataka kuwa mchekeshaji haya ni sawa," Alisema. 

Mulamwah alisema kwamba kazi ya muuguzi ni nyingi sana na hana wakati wa kutumia pesa zake licha ya wauguzi wengi kuwa na pesa.