Nyahunyo:Mtoto wa kaka yangu amekuwa akinirushia mistari

Muhtasari
  • Katika kitengo cha nyahunyo mwwanamke mmoja alitaka mtoto wa kaka yake apewe nyahunyo kwa kuwa na tabia ambayo haipendezi katika jamii
Dj_gregg254,Mbusi na Lion
Image: Radiojambo

Je kizazi cha sasa, kinafuata utamaduni ambao ulikuwa umeekwa na akina babu zetu, kwani jinsi mambo yalivyo na kuonekana ni kama wamesahau kanuni na utamaduni.

Katika kitengo cha nyahunyo mwwanamke mmoja alitaka mtoto wa kaka yake apewe nyahunyo kwa kuwa na tabia ambayo haipendezi katika jamii.

Kulingana na mwanadada huyo, mwanamume huyo amekuwa akimrushia mistari na hata kumsihi wafanye ngono.

"Nataka mtoto wa kaka yangu apewe nyahunyo kwani amekuwa akinikatia kwa muda mrefu sasa, nilimshauri aende akawakatie wasichana wengine lakini hasikii

Licha yangu kuwa shangazi yake, ananiuliza kama anaweza kusoma katiba, sio mimi tu peeyangu ambaye amekuwa akiniambia kwamba ananipenda pia alikuwa anamtaka dada yangu mkubwa," Alisimulia.

Je mwanamume huyo alikuwa na makosa kweli na alistahili kupew nyahunyo? au ni kizazi kimeoza?