Visa 28 zaidi vya coronavirus vyasajiliwa nchini na kusukuma idadi ya walioambukizwa hadi 649

Visa 28  zaidi vya Ugonjwa  covid 19  vimeripotiwa nchini na kufikisha  jumla ya  visa 649  tangu  ugonjwa huo kuripotiwa nchini .

Kati ya 28 hao  24 ni wakenya  ilhali  4 ni raia wa Tanzania . wagonjwa 10 ni kutoka Mombasa ,9 Nairobi 4 Migori ,2 Kajiado  na kisa kimoja kutoka kaunti za  Machakos ,Kiambu  na Homabay . Katika jiji la Nairobi ,visa  9 vilivyripotiwa vilipatikana katika mitaa ifuatayo;3 Embakasi,2 Kayole,1 Huruma ,1 South B na kisa 1 Kawangware . Umri wa watu walioathiriwa ni kati ya  miaka 11 na 81 . 17 ya waliopatiakana  na ugonjwa huo ni wanaume ilhali 11 ni wanawake .

Katibu wa utawala wa wizara ya Afya  Rashid Aman amesema mtu mmoja zaidi ameaga dunia na kufikisha 30 idadi ya watu ambao wameaga dunia hadi kufikia sasa . watu wengine 5 wamepona virusi hivyo na kufikisha 207 idadi ya waliopona ugonjwa huo .

Aman amesema makundi  ya maafisa wa afya kutoka wizara ya afya yametumwa katika kaunti za mipakani ili kuzisaidia kaunti hizo kukabiliana na virusi vya corona baada ya ongezeko la idadi ya watu wanaoambukizwa ugonjwa huo katika maeneo ya mipakani .

Kaunti ya Mandera imenufaika na msaada wa wizara ya afya  wa kuwafanyia watu vipimo vya corona  kabla ya matokeo kuletwa jijini Nairobi kwa tathmini .