Lakini utachukuliaje tukio la mwanamme kumkataa mwanamke eti kwa sababu mwanamke huyo ni bikra? Alex inadaiwa alipogundua kwamba Irene ni bikra alimuambia kwamba hayuko tayari kwa uhusiano kati yao .
Kulingana naye , hataki kuwa na mtu ambaye hajawahi kufanya mapenzi kwa sababu ni kibarua kigumu kuanza kumvunja mtu ubikra . Hatua hiyo imempa sana msonono Irene akishindwa atazungumza na nani kuhusu masaibu yake ., Amejikuta akijuta kwa nini alihifadhi ubikra wake hadi umri wake wa sasa wa miaka 24 kwani anasema wenzake wengi wa kike wamekuwa pia wakimfanyia kejeli kwamba bado yeye ni bikra na umri wake mkubwa .
Irene amesema kuanzia shule ya msingi amekuuzwa na maadili ya kidini n ahata shule ya upili hakutaka kufanya mahusiano na wanaume hadi alipomaliza chuo kikuu kwa sababu anavyofahamu yeye kwa ajili familia yake ni kumcha mungu sana ,ngono ni kitendo cha kufanywa wakati mtu yupo katika ndoa na amesalia na ukakamavu wa kujizuia kujiingiza katika majaribio . Ameshangaa ni vipi uamuzi wake huo unavyoweza kumrudi kwa kumfanya kuachwa na mwanamume ambaye alitarajia angekuwa mume wake . Alex maajuzi amerejea kenya kutoka Canada ambako alikuwa akisomea na walikuwa wakiwasiliana kwa njia ya mtandao na Irene kwa takriban miaka mitano.
‘ Alipogundua kwamba sijawahi kuwa na mwanamume alianza kunichukulia kama mshamba, dhana hiyo yake ilinikwaza sana’ anasema Irene
Ameongeza kwamba mpango wake wa hapo awali ulikuwa kusomea utawa ili awe nun lakini baadaye alibadilisha mawazo yake baada ya wazazi wake kumshawishi kivingine. Irene sasa anasema anajutia mbona aliacha kusomea utawa kwani hangejipata katika hali hiyo endapo wazazi wake wangemruhusu aendelee na mipango aliokuwa nayo . Anasema wazazi walimfanya kubadilisha mwazo yake kuhusu mkondo huo kwa sababu yeye ndiye mtoto wa pekee .