Hakuna asiyependa mashindano ya mitandaoni ambayo kila mara huweka moto mitandao ya kijamii kote duniani na Kenya haijaachwa nyuma katika baadhi ya challenges hizi nyingi .
Maajuzi kumekuwa na Vogue Challenge ambapo akina dada warembo na mastaa Kenya na kote duniani walitumia ukurasa wa kwanza wa jarida la Vogue kuziweka picha zao ili kuonyesha minato nayo kwa wote .
Challenge hiyo ilianzishwa na Salma Noor aliyesema kwamba aligundua watu wengi weusi hawakuwa wamewekwa katika ukurasa wa kwanza na jarida la Vogue .
“ Kilichonivutia sana kuanzisha hili ni kwa sababu hapakuwa na uwakilishi wa waytu weusi ,na baada ya kuibuka suala la ubaguzi wa rangi Amerika nilihisi challenge hii ilifaa kufanywa’ amesema Salma
Tazama picha za celebs wa Kenya ambao walishiriki challenge hiyo na ujiamulie ni yupi aliyefaulu kuivuruga ifaavyo .