Wafanyikazi wa KNH waanza mgomo kuhusu kucheleweshwa kwa nyongeza ya mishahara

Wafanyikazi wa hospitali ya kitaifa ya Kenyatta wameanza mgomo wao leo kuhusu kutotekelezwa kwa nyngeza ya mishahara yao .

Wafanyikazi hao walibeba mabango  walipokuwa wakindamana mbele ya hospitali hiyo  huku wakionekana kupuuza kanuni ya kutokusanyika sehemu moja kwa wakati mmoja ingawaje wengi walikuwa wamevalia maski .

" Hatutakubali SRC kutuzungusha’ mmoja wao alisema  wakisema wako tayari kwa lolote .

Katibu mkuu wa muungano wao Seth Panyako  amesema wameamua kuufanya mgomo huo kwa sababu RC imeamua kujifanya kana kwamba ndio taasisi pekee nchini .

" Pesa ambazo tunazitaka tayari zimetolewa na kuidhinishwa . hakuna kurudi nyuma .Tunaitaka SRC itoe barua kwa KNH ikiishauri kutulipa pesa hizo na kisha tuufutilia mbali mgomo wetu’ amesema Panyako

Panyako  amesema hazina ya kitaifa tayari imetoa shilingi milioni 601  ambazo bunge lilikuwa limeshaidhinisha .

"...  Tatizo la pekee ni kwamba SRC haitaka KNH kutekeleza nyongeza ya mishahara . hatutakuwa na mazungumzo yoyote hadi tupate barua kutoka kwa SRC .