Wageni wapewa wiki mbili kuondoka au wapate vibali vya kusalia Kenya

muteshi
muteshi
Kenya  imeongeza muda wa msamaha kwa raia wa kageni walio nchini bila vibali wakati huu wa janga la corona .

Mkurugenzi wa huduma za uhamiaji  Alexender Muteshi kupitia taarifa  kwa raia wote wa kigeni amesema wana wiki mbili kuondoka nchini .Muteshi amesema hatua hiyo imechukuliwa kufuatia kurejelewa kwa huduma za safari za ndege .

Amesema wale watakaoathiriwa  wanafaa kupanga kuondoka  Kenya katika kipindi cha iku 14  zijazo kuanzia septemba tarehe 14 au  wachukue vibali vya kuruhuisiwa kuendelea kuishi Kenya .

Mwezi Mei Muteshi  alitoa arifa ya kuwaagiza polisi kutokawakama raia wa kigeni walio nchini  kinyume cha sharia . Alisema idara yake ilikuwa imepokea barua nyingi zilizotaka kujua hali ya raia wa kigeni waliokuwa wakiishi nchini .