Wairimu Cohen apinga kesi yake kuunganishwa na ya Peter Karanja

wairimu
wairimu
Sarah Wairimu anayekabiliwa na mashtaka ya mauaji ya aliyekuwa mumewe Tob Cohen amepinga ombi la kuunganisha kesi dhidi yake na ile ya mfanyibiashara Peter Karanja kuhusiana na mauaji ya Cohen.

Upande wa mashtaka unasema kwamba kesi dhidi ya wawili hao zinauhusiano wa karibu ikiwemo jina la marehemu na saa katika stakabadhi za kesi.

Wawili hao wameshtakiwa kwa mauji ya Tob Cohen ambaye alikuwa bwanake Wairimu.

Hata hivyo, wakili wa Wairimu Phillip Murgor amekatalia mbali ombi hilo akisema kwamba hawajapa taarifa za mashahidi na hivyo hawana uhakikika ikiwa kesi za wawili hao zinafafa.

Karanja pia imepinga kujumlishwa kwa kesi hizo.

Upande wa mashtaka ulikuwa umesisiza kwamba kesi hizo ziwekwe pamoja kama ilivyo desturi ya kesi zinazohusiana.

Wairimu mwezi uliopita alikanusha kumuua Cohen. Baadaye aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni nne na hakikisho au shilingi milioni mbili pesa taslim.

Alitakiwa kuwasilisha mahakamani hakikisho kutoka kwa wazazi wake kwamba watamtunza kabla ya kuachiliwa.

Jaji Stella Mutuku pia alimuagiza Sarah kutowasiliana na ndugu wawili wa Cohen na kutokaribia biashara za Chonen, Tob Ltd.