Wajua mapato ya Messi ni maradufu ya Ronaldo? Orodha ya Mishahara ya Wanasoka 10 Bora Duniani

messi-compressed
messi-compressed
Ni wazi  kwamba watu wengi sana huthamini soka kwa kuwa unavutia donge noo  sana, ila baadhi ya mashabiki hawajui ni kwamba  mapato ya kila  mwanasoka hutofautiana sana kulingana na ubora wake  na ustadi wake kwa timu anayochezea.

Katika ulingo wa soka, Messi yupo kileleni kwa  wale wanaotiia kikapuni  mpunga mkubwa sana ambayo ni maradufu zaidi ya kile mshindani wake Ronaldo anapata kila mwezi.

Kulingana na ripoti iliyochapishwa na  L’Equipe,  nyota wa Barcelona Lionel Messi anaongoza  kutokana na kiasi kukubwa cha mshahara anayolipwa.

Mwajentina huyu  ambaye hucheza kama kiungo wa mbele ,  hutia mfukoni  kima cha  pauni milioni 8.3, hii ni takribani  shilingi milioni  957,874,833.95 kila mwezi.

Naye nyota wa Ureno, ambaye aligura Real madrid na kujiunga na Juventus analipwa kima cha pauni milioni 4.7 kila mwezi ambayo ni shilingi milioni  542,445,183.36.

Ronaldo ndiye mwanasoka wa pekee anayecheza kule Italiano ambaye amerodhoshwa kwenye 10 bora.

Hata hivyo, Hispania  inaongoza katika orodha hiyo wakiongoza huku watano kati yao wakichezea ligi ya La Liga.

Hii hapa ni orodha ya wachezaji 10 wa soka wanaolipwa donge nono kila mwezi kabla ya kutozwa ushuru:

1. Lionel Messi (€8.3 Million)

2. Cristiano Ronaldo (€4.7 Million)

3. Antoine Griezmann (€3.3 Million)

4. Neymar (€3.06 Million)

5. Luis Suarez (€2.9 Million)

6. Gareth Bale (€2.5 Million)

7. Philippe Coutinho (€2.3 Million)

8. Alexis Sanchez (€2.28 Million)

9. Kylian Mbappe (€1.73 Million)

10. Mesut Ozil (€1.6 Million).