Wakazi wa Lurambi wakashifu hatua ya mwanakandarasi anayeweka lami barabara

Wakazi wa eneo la Lurambi na Navakholo wamekashifu hatua ya mwanakandarasi anayeweka lami barabara ya kutoka Lurambi kwenda Navakholo hadi Bungoma kuondoa vifaa vyake vya kazi katika barabara hiyo kabla ya kukamilika

Wakiongozwa na Moses Musundi na Thomas Arasha wamesema matumaini yao ya kupata lami yamedidimia baada ya mwanakandarasi kuondoka na wamewataka wabunge wao Titus Khamala wa Lurambi na Emmanuel Wangwe wa Navakholo kuingilia kati na kuona kwamba barabara hiyo inakamilika.

Kwingineko

Wakulima wa miwa eneo la Mumias kaunti ya Kakamega wamesuta mgao wa bajeti wa shilingi milioni mia saba wakisema ni kidogo mno ikilinganisha na mahitaji ya sekta hiyo.