Maelezo hayo yametolewa huku wakenya wengine waliokwama Beirut ,Lebanon pia wakiishinikiza serikali kufanikisha kurejea kwao nyumbani .Serikali inatawaka wapate stakabadhi zifaazo kutoka kwa ubalozi mdogo nchini humo .
Balozi wa Kenya nchini India Willy Bett amesema wengi wa waliokwama nchini India kwa ajili ya janga la corona walikuwa wamesafiri kupokea huduma za matibabu ilhali wengine walikuwa watalii na baadhi yao walikuwa wanafunzi .
Hata hivyo watarejeshwa nyumbani kwa gharama yao kwani ndege ya KQ inatarajiwa kuwarejesha Nairobi Agosti tarehe 19 na watawasili Nairobi saa tatu kasorobo siku ifuatayo .
Nchini Lebanon ambako mlipuko katika mji mkuu Beirut ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 130 ,serikali ya kenya imethibitisha kwamba wakenya watatu walijeruhiwa katika tukio hilo .
Ms Halima Mohamud, balozi wa Kenya Kuwait ambaye pia anasimamia Lebanon amesema wakenya wote waliojeruhiwa wametibiwa na kuruhusiwa kuondoka hospitalini .