Wanakuonea wivu! Akothee amuambia Bahati huku akimtetea

Mwanamuziki Bahati amejipata katika meza ya kupigwa visu na wenzake na mashabiki lakini kuna mwenzake katika fani ambaye bado anamuunga mkono –Akothee.

Willy Paul maajuzi amemkosoa Bahati na hata kutilia doa talanta yake kumuziki ,lakini kothee ,mama ya watoto watano yupo upande wake  na amesema wanaomkosoa Bahati ni watu wanaomuonea kijicho kwa sababu ya mafanikio yake . Alimpongeza Bahati kwa kazi nzuri ikiwemo kuwa Baba ,mume na mwanamuziki .

 “ Umwashangaza wengi kwa hatua zako na majukumu unayobeba kama mzani ,lakini baadhi ya  mabaradhuli mtandaoni  wanaweza tu kuhesabu ni mara ngapi wapenzi wao wametoa mimba ….’ Akothe aliandika .

Akothee hakukomea hapo kwani aliongeza kwamba mafanikio ya Bahati ndio yanayomfanya kulengwa mtandaoni  na kwamba  anafaa kufurahia yote alioanywa kwa sababu ya muziki

“So just know that putting your family on clean limelight get ready to be admired, and it’s the only success that triggers jealousy, otherwise they will ignore you, your brand gets stronger when people talk about you   Keep doing what you are good at doing, they are not sleeping, it tells you they are watching   , they are among the 200k views in one day  , you are winning, @bahatikenya you have mad fans and support behind you my son, waoshe wanyorosheeeeee  , I am your number 1 supporter  @bahatikenya @diana_marua Nakupa _moyo link on my bio  ,”  aliandika Madama Boss

Wawili hao walitoa wimbo pamoja kwa jina  Nakupa Moyo,  ambao ni wimbo wa gospel  siku ya alhamisi wiki jana  na wimbo huo umepokeleewa vyema katika youtube na mashabiki wao .