Wanawake wawili Wajiua Gilgil

  Wanawake  wamejiua katika visa tofauti huko Gilgil .mmoja  alipatikana akining’inia mtini karibu na eneo la langa langa  ilhali mwingine alipatikana amejiua chumba mwake mtaani site .

 Mkusanyiko wa Habari  na Matukio Muhimu ...

Suluhisheni utata wa pesa za kaunti-Ruto

Naibu wa rais William Ruto amezitaka bunge na wizara ya fedha kusluhisha kwaharaka utata kuhusu kiasi cha fedha zinazofaa kupewa serikali za kaunti . Ruto amesema  masuala yanayozuia kutolewa kwa fedha hizo yanafaa kujadiliwa na uamuzi kutolewa haraka ili kuepuka kuathiriwa huduma kwa wananchi katika kaunti .

   IEBC yazuiwa kumwajiri afisa mkuu mpya

 Mahakama ya leba imezidisha muda wa agizo la kuzuia kuajiriwa kwa  afisa mkuu mpya wa tume ya IEBC .mahojiano ya waliituma maombi ya kazi hiyo yalifaa kuanza leo hadi jumatano lakini  hilo sasa halitafanyika .jaji Byram Ongaya  alitoa uamuzi huo katika kesi  iliyowasilishwa na chama cha mawakili dhidi ya IEBC ,mwenyekiti wa tume hiyo na mkuu wa sheria .

  Mfungwa aliyefariki katika gereza la Naivasha alipigwa

 Matokeo ya uchunguzi wa mwili wa mfungwa  aliyefariki katika gereza na naivasha  wiki jana yameonyesha kwamba    alifariki kwa ajili ya majeaha alipata baada ya kupigwa na kifaa butu . Simon gitahi mwenye umri wa miaka 35 aliaga dunia katika seli aliokuw amewekwa pekee yake baada ya kudaiwa kushambuliwa na maafisa wa gereza hilo.

Ukaguzi wa Ebola waendelea Malaba na Busia

Ukaguzi  wa ebola unazidi kufanywa  katika  maeneo ya mpakani ya busia na malaba  ili kuhakikisha kwamba walio na daalili za ugonjwa huo  kutoka uganada wanatengwa . Everline walela kutoka wizara ya afya  amesema pia wameweka ishara katika  maeneo ya umma ili kuhamisha umma kuhusu ugonjwa huo.

  Walimu wakuu waonywa  kuhusu kuchomwa kwa shule

Waziri  wa elimu George Magoha  ameonya kwamba hatua zitachukuliwa dhidi ya walimu wanaokosa kuwazuia wanafunzi kuziteketeza shule .alikuwa akizungumzia kisa kilichotokea katika shule ya Upili ya Uriri ambapo wanafunzia waliichoma shule yao baada ya kuzuiwa kuutzama mchuano wa AFCOn kati ya Kenya na Algeria .

  Usirauke kupiga foleni kupewa paspoti

   Huna haja  ya kurauka  kupanga foleni kuanzia saa tisa  usiku katika jumba la nyayo ili  kuibadilisha paspoti yako  endapo huna mpango wa kusafiri hivi karibuni . idara ya uhamiaji  imesema itaendelea kutoa paspoti za kisasa hata baada ya agosti kwani zoezi hilo ni la kuendelea .

Wasimamizi wa elimu watakiwa kufanya ukaguzi wa kila mara 

Wasimamizi wa elimu katika  kanda wameshtumiwa kwa kuzembea kufanya ukaguzi katika maeneo wanayosimamia .waziri wa elimu George Magoha  amesema  kuna haja ya kuzidisha doria hizo ili kuhakikisha kwamba hakuna nja za  kufanya udanganyifu katika mtihani wa kitaifa  na pia kuzuia visa vya shule kuchomwa .

 West Pokot yaanza kampeini ya chano dhidi ya Menengitis

    Kaunti ya  Pokot magharibi imeanzisha  kampeiniya chanjo dhidi ya Menengitis  kwa watu walio na umri wa mwaka moja hadi 29 .gavana John lonyangapuo  amesema kampeini hiyo inawalenga watoto na watu wazima laki tatu walio katika hatari ya kuambukizwa ugonjwa huo.

 Madaktari Kisumu warejea kazini

Madaktari huko Kisumu wameufutilia mbali mgomo wao  na kusaini mkataba wa kurejea kazini na serikali ya kaunti . mwenyekiti wa muungano wao katika eneo la Nyanza  Kevin Osuri  amrewaagiza madaktari kurejea kazini mara moja

 Wahudumu wa afya Taita watishia kugoma

    Wahudumu wa afya huko Taita taveta wametishia kufanya mgomo  kwa ajili ya kuchelweshwa kwa mishahara yao . mwakilishi wa  muungano wao Kelvin Odongo  amesema wamekuwa wakihangaika kila mwezi kwa ajili ya kucheleweshwa kwa malipo yao.

  Mtihani wa gredi ya tatu kuanza Septemba

   Wanafunzi wa gredi ya tatu  watafanya mtihani wa kitaifa  kwa mara ya kwanza kuanzia tarehe 16 hadi 20 septemba . Afisa mkuu mtendaji wa  baraza la kitaifa la mtihani Mercy Karogo  amesema mtihani huo utawawzesha kufahamu changamoto katika mfumo wa elimu wa CBC .matokeo yatatolewa mwezi oktoba .