Washirika wa Ruto wakimbilia mahakama kupinga mkataba wa ushirikiano kati ya Jubilee na Kanu

Washirika wa naibu wa rais William Ruto  wamewasilisha kesi kortini ili kupinga mkataba  wa ushirikiano uliotiwa saini kati ya Jubilee na Kanu .

Kesi yao inalenga kupinga makubaliano hayo ya baada ya uchaguzi ambayo yalitiwa saini Ijumaa iliyopita na kuwasilishwa kwa msajili wa vyama vya kisiasa na  Hillary Kosgei. Wakati uo huo, naibu katibu mkuu wa chama hicho Caleb Kositany  alimuandikia barua ya lalama msajili wa vyama vya kisiasa Ann Nderitu  akitaja kama yasio halali makubaliano kati ya chama cha Jubilee na kile cha KANU .

Kositany  amesema kamati kuu ys kitaifa inayosimamia Jubilee haikukutana ili kuidhinisha mkataba huo  na hivyo basi haufai kukubaliwa kwa mujibu wa sheria za vyama vya kisiasa .

Kositany amesema makubaliano hayo ni ukiukaji wa sheria kwani utaratibu ufaao wa kisheria haukufuatwa.  Siku ya Jumanne  jopo la kusuluhisha  mizozo ya kisiasa  lilikizuia chama cha Jubilee kutekeleza mkataba wake wa muungano na chama cha Kanu.