Watu 268 wapatikana na virusi vya corona- Aman

Watu 268 wamepatikana na virusi vya corona baada ya kufanyiwa vipimo na kufikisha watu 6941 walioathirika na virusi hivyo nchini.

Kati ya visa hivyo vipya hii leo, wakenya ni 159 huku raia wa Kigeni wakiwa 9.

Watu wengine 20 wameruhusiwa kuondoka hospitalini na kufikisha watu 2,109 waliopona.

Nairobi inaongoza na visa 175 huku mitaa ya Dagoreti North ikiwa na watu 34 na mtaa wa Kibra ikiwa na 29.

Watu 3 wamefariki kutokana na virusi hivyo na kufikisha watu 152 waliofariki kufikia sasa kutokana na virusi hivyo.

Kufikia sasa Kenya imewapima watu 176,059 kuhusiana na virusi hivyo.

Aman amesema asilimia kubwa ya watu waliofariki kutokana na virusi hivyo nchini walikuwa na matatizo mengine ya afya.

Mombasa imesajili visa 28,kaunti ya Busia ikiwa na visa 18 Kiambu 11, Kajiado 9, Migori 9, Uasin Gishu 8, Machakos 6, Narok (2), Makueni (1), & Muranga (1).