Watu 3 wakamatwa kwa utekaji nyara na kuitisha fidia ya shilingi 150,000 Meru

police
police
Watu watatu wamekamatwa kwa  utekaji nyara na kitisha fidia ya shilingi elfu 150 ili kumuachilia mateka wao huko Meru .

Patrick Kimathi, Joseph Karithi   na  Daniel Muroki   wote walio na umri wa chini ya miaka 30 walikamatwa baada ya ripoti ya  mtu aluyepotea kuwasilishwa kwa polisi .

Maafisa wa  DCI   wamesema ripoti hiyo ilikuwa imewasilishwa kwa kituo cha polisi cha Kangeta ,Meru juni tarehe 19  mwaka huu .

Makachero kwa ushirikiana na polisi kisha walianza oparesheni  iliyopigwa jeki na habari za ujasusi katika eneo la Kiutune ,Igembe ya kati  . Polisi hao walielekezwa katika msitu wa Njuri Ncheke  katika kijiji cha mpinda ambako washukiwa walionekana wakijaribu kutoroka  lakini wakakamatwa kwa usaidizi wa wananchi .

Watatu hao kisha  waliwaelkeza polisi katika kichaka kilichokuwa karibu ambapo  mateka wao aliokolewa baada ya kuzuiliwa katika eneo hilo kwa siku 14 .

Mwathiriwa alipelekwa hospitalini kwa uangalizi huku washukiwa wakizuiliwa na polisi  na vitu kadhaa kuchukuliwa katika eneo la uhalifu ili kutumiwa kama ushahidi .