Miezi mitatu baada ya Billnass kumpa pete ya uchumba mpenzi wake Nandy ,yaonekana wawili hao wamechukua hatua za haraka kujitosa katika safari ya ndoa iwapo safari ya Nandy kumpeleka ukweni Billnas ni jambo la kutafsiriwa kwa njia hiyo .
Nandy alimpeleka mpenzi wake mkoani Kilimanjaro kuwakutanisha na baba ,babu na bib yake . Katika picha walizoweka kwenye instagram wawili hao walionekana kufurahishwa sana na hatua hiyo mpya katika mahusiano yao .
Billnass amesema amefurahia sana mapokezi ya wapare akisema hakutaka kuondoka .
https://www.instagram.com/p/CCYBlQNgfvB/