Nyota huyo hata hivyo pia amegonga vichwa vya habari kwa msururu wa vidosho ambao amehusiana nao na kisha kuwaacha hoi kila anapopata mpenzi mwingine. Diamond sio mgeni kwa sakata na amepata umaarufu sana wa kuweza kukana madai ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake kadhaa nchini Tanzania. Hawa hapa ni baadhi tu ya wanawake wanaojulikana kuwahi kuwa na uhusiano na Diamond ingawa amekuwa akikana kuhusika katika mahusiano yoyote na baadhi yao.
Zari Hassan
Mapenzi kati ya Diamond na Zari yalishika kasi kuzungumziwa kote Afrika. Walikuwa kilichotajwa kama ‘The altimate power Couple’ na kila mtu alitaka kuwa kama wao. Diamond alikuwa katika kilele cha taaluma yake ya muziki na Zari amefahamika sana kwa mafanikio yake katika biashara.Kiliingia mchanga kitumbua chao wakati Zari alipoushangaza ulimwengu kwa kudai kwamba Diamond alikuwa na uhusiano wa nje ya ndoa yao. Diamond na Zari walifanikiwa kupata watoto wawili Latifa Dangote na Prince Nillan.
Hamisa Mobetto
Uhusiano wa Hamisa na Diamond umeghubikwa katika usiri mkubwa lakini matokeo yake yamekuwa uvumi mrefu na sakata ya mara kwa mara. Kilichofichuka baadaye ni kwamba wawili hao wana mtoto Dylan. Hamisa aliwahi pia kujitosa katika muziki lakini hakuweza kupata mafanikio kama ya Diamond .
Tunda Sebastian
Tunda ni staa mwingine wa Tanzania ambaye amehusishwa na uhusiano wa kimapenzi na Diamond. Kipusa huyo ana urembo wa kuvutia na huwezi kumlaumu Diamond kwa kujipata katika mikono yake na cheche za mahaba ya mrembo huyo.
Wema Sepetu
Wema Sepetu imeripotiwa alikuwa mpenzi wa Diamond kwa muda mrefu na imekuwa vigumu sana kwake kujiondoa kabisa kutoka maisha ya msanii huyo. Wawili hao awali walikuwa wakionekana pamoja lakini katika siku za hivi karibuni, hawajakuwa wakitangamana kama ilivyokuwa miaka minne iliyopita .
Shaddy Boo
Kipusa huyu mnyarwanda ilidaiwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Diamond kisiri lakini kwa sababu mapenzi ni kama kikozi, hayawezi kufichika, baadaye yote yalijulikana. Wakati Fulani aliwahi kuweka picha mtandaoni akisema alikuwa ametekwa kabisa na mapenzi kwa msanii huyo .
VJ Penny
Muimbaji Penny alikuwa mpenzi wa zamani wa Diamond na hata walikuwa wamepanga kufunga ndoa mwaka wa 2013 kabla ya mambo kutibuka. Inaaminika wana mtoto lakini pia kuna uvumi kwamba huenda wawili hao wana ujamaa na hivyo basi kufanya kuwa vigumu wao kuonekana .
Tanasha Dona
Tanasha ndiye wa hivi punde kutengana na Diamond ingawaje watu wengi bado hawajaamini kwamba Diamond ameachana na Tanasha baada ya kutoa wimbo wao pamoja hivi karibuni . Jumbe anazotuma Tanasha katika mitandao ya kijamii zinaashiria kwamba huenda penzi lao liliingia mchanga .Je ni yupi sasa atakayefuata katika orodha ya msururu wa wapenzi wa Simba?