Who’s Next? Jeshi la Ruto Bungeni lapatwa na hofu baada ya washirika wake senate kufurushwa

Baada ya kuondolewa kwa washirika wa naibu wa rais William Ruto katika nafasi za uongozi wa senate ,washirika wake katika bunge la kitaifa sasa wapo  katika hali ya wasi wasi kwani  huenda ndio watakaolengwa .

Den Duale ,Ben Washiali na Kimani  Kimani Ichung'wa  wapo katika hatari ya kufurushwa katika nyadhifa za uongozi bungeni   baada ya kushtumiwa kwa kutokuwa waamonifu kwa kiongozi wa chama chao cha Jubilee Rai Uhuru Kenyatta. Baada ya kufaulu kutekeleza mageuzi  katika senate  washirika wa rais Uhuru Kenyatta sasa wamepata ujasiri wa kuzidisha adhabu yao hadi bungeni  na imeibuka kwamba mkutano wa wabunge wa Jubilee huenda ukafanyika tarehe 2 au 6 Juni .

Rais Uhuru Kenyatta analenga kunadhifisha usimamizi wa mabunge ypote ili kurahisisha utekelezaji wa jenda yake anapokaribia kumaliza muhuma wake mwaka wa 2022 . Ruto na viongozi katika mrengo wake wameshtumiwa kwa kuendeleza siasa za kumrithi rais Uhuru Kenyatta na kuhujumu jitihada za rais kutekeleza ahadi nyingi za maendeleo alizotoa kwa wakenya mwaka wa 2013 na mwaka wa 2017 . Washiali ambayeni  kiranja wa walio wengi bungeni ,naibu wake Cecily Mbarire na mwenyekiti wa kamati ya bajeti Kimani  Ichungwa,  ni miongoni mwa wanaolengwa endapo  Jubilee italenga kuendeleza msururu wa kuwaondoa washirika wa Ruto katika uongozi wa bunge.

Ingawaje jina lake limetajwa kwa wanaoweza kufurushwa kama kiongozi wa wengi bungeni ,Aden Duale amekuwa akituma jumbe za kukinzana wakati mmoja akieleza kwamba yupo nyuma ya rais Kenyatta na haijabainika endapo chuma chake kipo motoni .