William Ruto akubali kuunga mkono Wanyama royal charity cup

Naibu wa rais William Ruto amekubali kuunga mkono kiungo wa Harambee stars katika kuendeleza mpango wake wa Wanyama Royal Charity Cup. Mashindano haya yalianzishwa na Victor wanyama na nduguye mkubwa McDonald Mariga mwaka 2018.

Wanyama royal charity cup jukumu lake kubwa ni kuinua talanta mtaanii pamoja na kusaka vijana walio na umri usiozidi miaka 16.

"Tunaunga mkono jaribio la kusaka talanta, kukuza vipaji pamoja na kuzawadi ujuzi wa vijana ili waweze kujiunga na wana michezo maarufu ulimwenguni. Kukuza idara ya michezo nchini kwa kuwapa wachezaji wetu rasilimali wanazohitaji ni mojawapo wa nguzo kuu za kuhakikisha vijna wanabobea maishani mwao kwa kujipatia riziki ya kutosha."