Yote yaliyofichwa kuhusu marehemu Bob Collymore !Juliani afunguka

Mwanamziki freshi sana Juliani alifunguka kuhusu changamoto ya maisha yake na kuzungumza mwanzo mwisho kuhusu uhusiano wake na marehemu Bob Collymore .

Urafiki wa Bob Collymore na Juliani ulikuwa wa chanda na pete kiasi ambacho alikuwa miongoni mwa wageni wachache waliohudhuria harusi ya Marehemu Bob  na mke wake Wambui jijini Naivasha.

Miezi baada ya kifo chake Collymore,mwanamziki Juliani alifunguka kuhusu kiasi ambacho kifo chake Bob kilimuumiza roho na kusema,

 “YOU KNOW WHEN YOU ARE DOING THINGS PEOPLE SEE LIKE YOU ARE GOING CRAZY. BUT ONE NEEDS SOMEONE TO AFFIRM THEM THAT THEY ARE FINE. THIS IS THE ROLE BOB COLLYMORE PLAYED ON MY END,” Juliani aliambia vyombo vya habari.

Kifo chake Collymore kiliwasikitisha wengi na ilikuwa wazi kuwa nchi yote iliomboleza kifo chake.

Zaidi ya hayo,Juliani alisema kuwa,Marehemu Collymore alikuwa mtu ambaye angekusaidia wakati wowote una matatizo.Ama kwa hakika akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki.

“YOU KNOW THOSE KIND OF PEOPLE WHO IN CASE YOU GET INTO SOMETHING THEY ARE THE FIRST ONES TO LOOK UP AND THEY WON’T LET YOU. I COULD TELL HIM BOB SEND ME KSH 1K AND WOULD DO SO WITHOUT PROBING A LOT.”

Aisee!ni wazi kuwa marehemu Collymore alikuwa binadamu bora sana na wengi wanamkosa.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.